Тексты и переводы песен

Penseli

Ah rafiki ndugu na jamaa zangu wanalalamika
Msamaria wa leo amebadilikaga
Facebook yuko hewani kila muda utamuona
Hatakujibu na hata ukiandika
 
Ah wengine wanadai
Aliniomba namba whatsapp nikanyima
Hajui kwamba ni hatari
Hata simu ya kuchat naazima
 
Wengine ati nawasahau
Wengine ati nawadharau
Sababu superstar wa mda mdogo
 
Ooh wamesahau mziki wa Abuja
Ni michosho michosho tu
Natoa changu mfukoni
Siingizi kitu walahi
 
Ah najihisi raha
Naposkia nyimbo zangu kitaani
Ila roho inauma
Napo guza mfukoni aah
 
Tararara raa..Tararara raa
Wanafunzwa na umaarufu wangu
Tararara raa..
Oooh nisaidie Maulana
 
Mara rafiki anichukie
Anaponiomba vocha nisipompatia
Hataji Mungu aninunie
Pale anaponibeep nisimpo mpigie
 
Wana mateja wanitinge
Nikirudi nyumbani Nyakara
Wanigonge gonge ngumi
Kisa wamekuta ufukoni sina hela
 
Msamaria na meneja
Wenye pesa nyumba na gari kali
Jamani vile sio vyangu
Sina hata baiskeli natembea kwa mguu
 
Shabiki haamini
Pale tunapokutana
Anitegemea kuona mng'aro
Kulingana jinsi navyojulikana
 
Ah mziki wa Buja haulipi kiufupi
Meneja wangu anajituma
Ili aone kama nitatoboa tundu
Niwe kama wengine
 
Ila lala
Tatizo ni copy za studio za utani
Na tarara
Na nyimbo feki feki ndo zimezagaa
 
Najihisi raha
Naposkia nyimbo zangu kitaani
Ila roho inauma
Napo guza mfukoni aah
 
Tararara raa tararara raa
Oooh tantarara tararara raa
Eeeh Mola wangu nisaidie
Tararara raa
Heart ya mwenzetu inaumia
Tararara raa tararara raa
 

Понравилась песня? Будем очень благодарны, если вы расскажете о ней друзьям:



Послушать песню и посмотреть клип "Penseli"

Видеоклипы к песне подбираются автоматически сайтом youtube.com. Отказ от ответственности

Текст песни Diamond Platnumz Penseli предоставлен в ознакомительных целях для личного развития.