Тексты и переводы песен

Ongeza

Mmmmh....
(Ayo Lizer)
 
Mi kwako sikuingia miguu
Mikono hadi kichwa
Kiufupi mazima
Nikiamini wa kufa kuzikana
 
Yaani hoi sio nafuu
Mututi kabisa hata mashaka sina
Ukiamini
Utatengwa na Maulana
 
Mvumilivu hula mbivu
Nimengoja mpaka zikaoza
Naambulia maumivu
Ningali sina wa kunipoza
 
Sijui yangu stahimilivu
Kunyenyekea waniponza
Napambania utulivu
Mwezangu chuki unaikoza
 
Sikukufuta tu machozi
Ulipolia nililia na wewe
Sasa mbona wanilipa majonzi
Yaani stress mapombe mi nilewe
 
We ndo wangu Yesu Mkombozi
Sa mbona Petro unaniacha mwenyewe
Nikose usingizi na njozi
Ndo ufurahi okay sawa
 
Si unataka nitukanwe
Ongeza ongeza bado
Nidhalilike
Ongeza ongeza bado
 
Nikose pa kuificha sura
Ongeza ongeza bado
Marafiki wanicheke, waning'onge ada
Ongeza ongeza bado
 
Mmmh kisichokuua hukukomaza
Ati ikiwa sikani huo msemo nakataa
Maana jua linapoangaza na sina afadhali
Mi kwangu ni mabalaa
 
Oooh najitahidi kumsinga mwali
Ila somo ananikataa
Oooh penzi letu si la kibatari
Anayamwaga mafuta taa
 
Kutwa ni vurugu ndani
Purukushani hapakaliki
Roho inaniuma yaani
Kwanini sa tunagombana sweetie
 
Oooh njema gani
Niambie labda nitende kipi? (Aah)
Hata pa kucheka hunnie
Ati utani unapanic
 
Naelewa riziki mafungu saba
Na la kwangu sita
Naelewa sikutoshi labda
Kukuridhisha
 
Sikukufuta tu machozi
Ulipolia nililia na wewe
Sasa mbona wanilipa majonzi
Yaani stress mapombe mi nilewe
 
We ndo wangu Yesu Mkombozi
Sa mbona Petro unaniacha mwenyewe
Nikose usingizi na njozi
Ndo ufurahi okay sawa
 
Si unataka nitukanwe
Ongeza ongeza bado
Nidhalilike
Ongeza ongeza bado
 
Nikose pa kuificha sura
Ongeza ongeza bado
Ndugu jamaa wanicheke, waning'onge ada
Ongeza ongeza bado
 
Aah nikose pa kuificha sura
Waning'onge ada
 
(Wasafi)
 

Понравилась песня? Будем очень благодарны, если вы расскажете о ней друзьям:



Послушать песню и посмотреть клип "Ongeza"

Видеоклипы к песне подбираются автоматически сайтом youtube.com. Отказ от ответственности

Текст песни Diamond Platnumz Ongeza предоставлен в ознакомительных целях для личного развития.