Тексты и переводы песен

Lala Salama

Lala salama
Matatizo, chuki, lawama
 
Ukilala lala salama, kumbatia picha yangu
Na kama ukinikumbuka sana nipigie simu yangu
Uki-ukilala lala salama, kumbatia picha yangu
Matatizo, chuki, lawama vumilia mpenzi wangu
 
Najua wivu ndo mapenzi, ila chunga usizidi
Si unajua kwako sijiwezi, ila dhiki mmebidi
Mi nilitamani sana mi kuwa nawe
Tuwe wote usiku na mchana
Kilichonifanya mi nipagawe
Sina chochote cha kuwalisha wana
Niliupokea kwa unyonge msiba wa kaka Bonda
Ile barua yako ya mwisho ilinitonesha vidonda
Usije nilali kipenzi changu
Ukadhani nimekumbwa na pepo la starehe
Mambo bado magumu kwangu
Afadhali hata ya jana, ya kesho niombee
 
Ukilala lala salama, kumbatia picha yangu
Na kama ukinikumbuka sana nipigie simu yangu
Uki-ukilala lala salama, kumbatia picha yangu
Matatizo, chuki, lawama vumilia mpenzi wangu
 
Ile “kua uone”, nilidhani maghorofa
Ah aa kumbe mwana ukome, hakuna cha kuokota
Mi bado nakaza moyo changu kipenzi
Ila naumia kwa kuwa mwenyewe
Natamani ila siwezi, nazitafuta nije kula na wewe
Msalimu mama nyumbani, usiseme kama nahenya
Tai, mfiche mpe imani, karibu ntakuoa chema
Usije nilali kipenzi changu
Ukadhani nimekumbwa na pepo la starehe
Mambo bado magumu kwangu
Afadhali hata ya jana, ya kesho niombee
 
Ukilala lala salama, kumbatia picha yangu
Na kama ukinikumbuka sana nipigie simu yangu
Uki-ukilala lala salama, kumbatia picha yangu
Matatizo, chuki, lawama vumilia mpenzi wangu
 

Понравилась песня? Будем очень благодарны, если вы расскажете о ней друзьям:



Послушать песню и посмотреть клип "Lala Salama"

Видеоклипы к песне подбираются автоматически сайтом youtube.com. Отказ от ответственности

Текст песни Diamond Platnumz Lala Salama предоставлен в ознакомительных целях для личного развития.