Diamond Platnumz — Haunisumbui

Diamond Platnumz Haunisumbui

Текст песни

(Ayolizer)
 

Si kokoko si kandambili

Yaani vyote havikupendezi

Mwana ngoko usonawili

Tope bin uterezi

 

Utaishia kututabiri

Tubomoke inasonga miezi

Mola ameshatakabiri

Usijichoshe halivunjiki penzi

 

Ona! umekosa nuru

Umekosa bahati huna

Unaitwa kunguru

Ukifika wananuna

Ndo ndo ndo mwana chururu

Asiye mbuzi wataka chuna

Mengine nisikufuru, mmmh

 

Hazikukai maskara

Wala make up zinakushuka

Uso umekuparara

Mwili shock up, zimetenguka

Uso sauti ya stara

Kwa kudeka unawehuka

Jibwa koko la Mbagala

Unabweka na kubwetuka wala!

 

Wala haunisumbui wala

Wala haunisumbui wala

Wala haunisumbui wala

Wala haunisumbui wala

 

Na hizo post mara kubebana

Mara eti mnabusu mtamaliza bando

Unaowatuma kunitukana

Siogopi mashushu me wala michambo

 

Kutwa kwa mapage feki

Kama lokole linahusu...?

Mkwe akutaki eti

Mwenzangu pole mbona kuntu

 

Vimeseji kujitumisha

Kwa ndugu zangu marufuku

Nyota imekufubika

Usifosi umaarufu

 

Upepo wa kisulisuli

Unakuchukuwa na nuksali

Tanga lipulipuli

Wanakununua kwa mizani

Kwangu mpambe shughuli

Najiashua burudani

Na toto nzuri nzuri

Nimelitua tuli ndani ii

 

Ona umekosa nuru

Umekosa bahati huna

Unaitwa kunguru

Ukifika wananuna

Ndo ndo ndo mwana chururu

Asiye mbuzi wataka chuna

Mengine nisikufuru

Usiye wa shaba wala chuma

 

Wala haunisumbui wala

(Wala hamunikondeshi)

Wala haunisumbui wala

(Mujipost mainstagram)

Wala haunisumbui wala

(Wala hamunitetereshi)

Wala haunisumbui wala

(Waaalah)

 
(Wasafi)
 

Клип «Haunisumbui»

Видеоролики хранятся и модерируются сервисом YouTube. Отказ от ответственности

Заказать перевод Прислать свой вариант перевода

Текст песни Diamond Platnumz Haunisumbui предоставлен в ознакомительных целях для личного развития.